Jumanne, 4 Novemba 2014

UHUSIANO



JINSI YA KUFANYA ILI KURUDIANA NA MPENZI WAKO WA ZAMANI-3

Leo tunaendelea na hatua ya 4 na ya mwisho katika muendelezo wa njia au jinsi ya kufanya kurudiana na mpenzi wako wa zamani. Kupata hatua za mwanzo bofya http://eliasadolf.blogspot.com au kwenye facebook page inayoitwa eliado love stories.
HATUA YA 4: WASILIANA NAE.
Kumbukuka mpenzi wako alipokuacha, alikuona na kukuchukulia wewe ni mkosaji, mdhaifu na usiyejiheshimu. Lakini kwa kitendo chako cha kumtomtafuta kwa mda, lazima ashangae na kujiuliza maswali mengi juu yako. Je, amepata mwingine mzuri zaidi yangu? Je hanipendi tena?........ 
Hapa ataanza kusahau madhaifu yako yote na kuanza kukukumbuka vitu vizuri ambavyo ulikuwa ukimfanyia. Ataanza kukumbuka vitu vizuri ulivyo navyo wewe. Pindi utakapowasiliana nae, hakikisha unaongea nae na ikibidi mnaonana. Vifuatavyo ni vitu vya kuzingatia kabla ujawasiliana nae.

  1. Umehakikisha hujawasiliana nae zaidi ya mwezi  
  2. Umefanya mabadiliko katika maisha yako
  3. Una uhakika kuwa kurudiana nae ni uamuzi sahihi 
  4. Umekubaliana na sababu za nyie kuachana
  5. Una uhakika kuwa hata kama hatokubali kurudiana na wewe utaendelea na maisha yako ya furaha.
NJIA ZA KUWASILIANA NAE
(a)    Barua pepe
Kwa kuwa barua imepitwa na wakati katika kizazi hichi cha digital, unaweza kutumia barua pepe au mitandao mingine ya kijamii. Barua pepe lazima iwe na malengo matatu
  1. Kumfanya mpenzi wako aolewe kuwa umekubaliana na hali ya wewe na yeye kuachana. Na kwamba pia haikuwa kitu kibaya
  2.   Kuomba msamaha sehemu zote ulizokosea
  3.   Kumjulisha kuwa kuna mambo mazuri yanaendelea kukutokea katika maisha yako, mfano kupata kazi, kununua gari. Ila usimweleze sana ili awe na hamu ya kujua zaidi nini kimetokea kwenye maisha yako mara baada ya kuachana.
(     (b)   Ujumbe mfupi wa maneno
Sms itume  mara baada ya kutuma barua pepe. Pia unaweza usitume barua ukatuma sms moja kwa moja, kwa sababu wewe ndo unamjua zaidi mpenzi wako tumia njia yoyote ambayo utakayoona ni sahihi au zote kwa pamoja.
Kitu cha kuzingatia hapa unapowasiliana nae usizungumzie moja kwa moja kuhusu uhusiano wenu. Pia epuka kutuma ujumbe usiojitosheleza. Ujumbe ambao utapunguza yeye kujibu kitu kwa mfano
“mambo” “i miss you” “upo” na zingine na kifupifupi.
Kamwe usizungumzie kuhusu hisia na mapenzi au unataka kurudiana nae kwa mfano
“ i love you” “nateseka sana juu ya penzi lako” i want you back na zingine unazozijua.
Epuka kusema kitu kibaya kwenye meseji kama “ watoto wako wanakukumbuka sana, ulifanya makosa sana kuwaacha wateseke” au “ kama usingekuwa na tamaa, naamini tusingeachana”
Ila unaweza kuandika vitu vifuatavyo katika ujumbe wako wa mneno
“ leo naangali filamu mpya ya Dimond na Wema, imenikumbusha pindi tukiwa pamoja.
Mkumbushe vitu ambavyo mlishawahi kufanya pindi mlipokuwa pamoja kwa mfano
“ Dah, nimekumbuka siku tulivyokwenda Marangu waterfalls, siku ile ilikuwa ya furaha sana. Nafurahi tulifurahia”au “Mambo, leo nimepika wali samaki nimekumbuka jinsi ulivyokuwa ukinipikia”.
MUOMBE MUONANE
Baada ya kuwasiliana nae muome muonane ana kwa ana, ila usimwambie kuwa ni siku ya kufanya mapenzi, bali ni siku ya kuonana tu. Usimwoneshe kuwa unataka kurudiana nae. Onesha kuwa unataka mtoke kama marafiki tu lakini unaweza kufanya vitu vya kumvutia mnapokuwa pamoja. 
Mfano kumkumbatia. Njia nzuri hapa ni kumkaribisha chakuala au kuenda naekuanagalia sinema au sehemu yoyote yenye burudani.
Baada ya hapo siku ingine lazinma takutafuta na kukuomaba muonane hapo usifanye makosa na kuzungumzia mambo mabaya yaliyowafanya muachane, zaidi tazama mbele anza upya. 
Siku hii ni nzuri kama mtalimenya tunda na kukumbushia enzi zenu. Amini sasa ni wako mpende kama zamani na sahau yaliyopiata wazungu wanasema “there is no point digging old graves when you want  to start a new life”....
KWA LEO TIUSHIE HAPA, ILA USIKOSE TOLEO LIJALO LINALOHUSU VITU VYA KUFANYA ILI USIACHANE NA MPENZI WAKO.

0 comments:

Chapisha Maoni