JINSI YA KUMFANYA MWANAMKE AKUPENDE
Wapo wanaume wanaozani kuwa kuna njia za kutongoza la hasha hakuna formula maalumu
za kutongoza kwa kuwa wanawake wanatofautiana kuanzia tabia, umbo na mwenekano.
Ila kuna njia za kumfanya mwanamke akupende, akutake, akutamani na ikibidi
akutongoze kabisa. Hivi unajisikiaje mtoto wa kike akikuambia anakupenda au kwa
lugha rahisi akikutongoza.? Bila shaka utajisikia kidume tena kidume cha mbegu.
Nsikuchoshe ngoja nikupe njia.
( 1. JIJALI NA KUJIPENDA MWENYEWE
Bila shaka muonekano wa nje ni muhimu zaidi kuliko kitu
kingine chochote. Ebu nikuulize swali hivi kuna mwanaume anayeweza kuvutiwa na
kumtongoza msichana mchafu anayenuka na kuvaa ovyo ovyo? Kama jibu ni hapana
ndivyo ilivyo kwa wasichana pia hakuna mwanamke anayependa au kuvutiwa na
mvulana anaevaaa ovyoovyo, hasiyependa kujitunza na kujithamini. Kuvaa vibaya,
kuwa mchafu ni ishara ya ushamba na siku zote ushamba unawaboa kinadada. Upo
hapo sio unanitolea mimacho tu mwanaume mzima unavaa mlegezo. Cha msingi ni kujijali
mwenyewe kuanzia chakula, malazi na mavazi. Sasa kama unakula hovyo hovyo
lazima utaonekana ovyo ovyo (garbage in, garbage out).
Fanya mazoezi kuweka mwili wako vizuri . kumbuka mwanamme aliyejengeka misuli
vizuri ni kivutio kwa wadada na kwa kuwa wanaongozwa na hisia basi hata kwenye
tendo la ndoa huisi kufikishwa kileleni na wanaume wenye afya njema. (sasa sio
ukapige jimu ambazo hazijapimwa ukajazia upande mmoja wa kifua na kwingine
ukabaki njiti mimi simo) Lakini nazani unanielewa fanya mazoezi mara kwa mara.
2. KUWA MTU WA WATU
Usipende kukaa mwenyewe jitahidi kujichanganya na watu wa
aina mbalimbali hasa wasichana warembo na kwa kufanya hivyo utapata na
kujifunza njia za kuishi na wasichana utajua nini wanapenda na nini hawapendi
kufanyiwa.Waone wasichana kama rafiki zako lakini kuwa makini usiwe mwongeaji
sana maaana utakuwa used and boared. Msichana yeyote anavutiwa na kupenda
mvulana au mwanaume anayeshirikiana na watu wa aina mbalimbali na hii ni ishara
kuwa hatokuwa mpweke pindi mtakapo kuwa kwenye mahusiano .
(
3. KUJIAMINI NI SILAA
3. KUJIAMINI NI SILAA
Linapokuja suala la kujiamini hata mwanaume awe mbaya kiasi
gani kama anajiamini lazima atakuwa kivutio kwa wasichana wanaokutana nae.
Wasichana siku zote wanapenda ulinzi, mtu ambae atakuwa kinga yake sasa ushawai
kuona mlinzi hajiamini? Kujiamini ni ngao kwa sabababu wanaume wanafanana kwa
vitu vingi kwa mfano mavazi yao huwa hayawatofautishi sana, kwa hiyo kwenye
kundi la wanaume wanaovaa sawa lazima mwanaume anayejiamini ataonekana wa
kipekee zaidi. Kujiamini kunamfanya mwanamke ajihisi kuwa salama pindi atakapo
kuwa na wewe kwa hiyo wanavutiwa sana na wanaume wanaojiamini tupilia mbali
sura na uhandsomboy. Badilika ndugu jiamini na kujikubali jinsi ulivyo.
4. ONESHA HISIA ZAKO KWA UMPENDAYE
Kwa mila na tamaduni zetu za kiafrika hata mwanamke awe
anakupenda vipi ni ngumu kusema kuwa anakupenda. Cha msingi kama umegundua kuwa
anakupenda na wewe unampenda ni vizuri ukafunguka kuliko kukaa kimya kwani
kukaa kimya kutamfanya aone huna hisia na yeye hivyo kuwa mbali na wewe. Ila
kuwa makini sio kwa sababu anavutiwa na wewe basi ukamtongoza tuu ata kama sio
chaguo lako hiyo ni dhambi kubwa. Wakati mwingine msichana anaweza kuvutiwa na
wewe kwa jinsi ulivyo na confidence, very attractive and sexuality lakini
akakuchukulia kama rafiki wa kawaida tu kwa hiyo kwa kuonesha hisia zako kwake
utakuwa umevunja mipaka ya urafiki na kuingia kwenye mahusiano...
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjE76D_wdUqnAKw_V5wyjmOL_c7Gk9rslbgeA6pBLKlANerhfDqkatDd3pDBb5UzlyjZSqEy0bcSHaux1eqduT7bkLjS_eBzSrRP7aX3V_j9iFSdJAKiEh0VpvY-vsS-CSSlPCAniAHrF8/s1600/lv.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjE76D_wdUqnAKw_V5wyjmOL_c7Gk9rslbgeA6pBLKlANerhfDqkatDd3pDBb5UzlyjZSqEy0bcSHaux1eqduT7bkLjS_eBzSrRP7aX3V_j9iFSdJAKiEh0VpvY-vsS-CSSlPCAniAHrF8/s1600/lv.jpg)
Leo tuishie hapa next time tutaangalia
DALILI ZA MWANAMKE ANAYEKUPENDA. Don’t misss.....
0 comments:
Chapisha Maoni