Jumanne, 7 Oktoba 2014

DARASA HURU



ZIJUE AINA NA MAKUNDI YA WATU DUNIANI
Tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa kuna watu wa aina tofauti hapa duniani. Ni vizuri kujijua upo katika kundi gani na kama ni kundi baya basi kuna hatua za kuchukua kujiondoa katika kundi hilo.
1.      WATU AINA YA SANGUIN
Hili ndilo kundi kubwa la watu, ni kwamba hawa ni watu ambao hawana maneno mengi. Hata uwezo wao pia wa kupambanua mambo ni wa kawaida, wanapenda kwamba wanapoongea jambo uwe una msikiliza. Pia watu hawa ni maarufu wa kueleza mipango yao ya kimaisha ingawa baadhi yake huwa haifanikiwi. Wale watu wanaopenda kuigiza na kuchekesha wapo kwenye kundi hili. Pia watu aina ya Sanguini ni watu wenye roho nzuri sana. Kama ni mwanamke yupo kwenye kundi hili basi ni ngumu sana kumshawishi kwa maneno na kufanikiwa kumpata.
2.      WATU AINA YA MELANCOLIN
Hawa ni watu wenye uwezo mkubwa wa kupambanua mambo na kama wapo darasani huwa wana uwezo mkubwa wa masomo magumu kama sayansi na hesabu. Watu wa kundi hili huwa na huruma sana lakini wanasumbuliwa na tatizo la kutojiamini ingawa wanachokisema mara nyingi huwa na mashiko. Baadhi yao huwa wanakata tamaa haraka na huwa hawapendi kuvunja sheria. Pia ni wagumu wa kusahau lakini wepesi wa kuadhibu na kuhukumu. Ni wasiri mno japo uongozwa na uaminifu na ukweli.
3.      WATU AINA YA FLAGMENTIC
Watu wa kundi hili mara nyingi hawana msimamo na ni wepesi wa kuharisha mambo, kwa mfano kama ni mwanamke anaweza kuamua kupika wali lakini akimaliza tu kupiga mboga anabandika sufuria la ugali. Ni wadadisi sana na wana uwezo mkubwa wa kukaa na siri moyoni. Wanaweza kujenga hoja na wakati mwingine kubadili ukweli kuwa uwongo au uwongo kuwa ukweli. Watu wa kundi hili wanaumizwa sana na mapenzi na wengi wao hawapo kwenye ndoa ni wepesi na kuacha na kutoa talaka.
4.      WATU AINA YA COLERICK
 Watu wa kundi hili wanapenda sana kutawala wenzao ingawa uwezo wao wa kiakili ni wa  kawaida. Watu wa kundi hili wanajiamini kupita kiasi, hawapendi kuongea ongea wala kucheka cheka hovyo. Hili ni kundi la watui matajiri sana duniani ambao hata wakikusaidia ni kwa malengo ya kupata faida zaidi. Watu wa namna hii mara nyingi hawapendi sana starehee.
KAZI KWAKO KUJUA UPO KUNDI GANI.........Usikose DARASA HURU la kesho.

0 comments:

Chapisha Maoni