Jumapili, 2 Novemba 2014

UHUSIANO



HATUA ZA KUFUATA KURUDIANA NA MPENZI WAKO WA ZAMANI-2.

 
Ndugu wasomaji wa makala zangu za uhusiano leo tunaendelea na hatua za kufuata ili kuweza kurudiana na mpenzi wako wa zamani. Hataua ya kwanza nilizungumzia makosa ya kuepuka ukitaka kurudiana na mpenzi wako ikiwa ni pamoja na;
(       (a)   kumpigia simu au kutuma sms kila mara
(       (b)   Kamwe usimwombe msamaha.
(c)  Usikubali kila kitu anachotaka
(d)   Usiendelee kuonesha kuwa unamjali
(e)   Usichukie ukigundua yupo na mtu mwingine.

Kama ulikua hujasoma hatua ya kwanza, basi isome kwenye blog hii kupata mtiririko mzuri.

Leo tuendelee na na hatua ya pili na ya tatu.
HATUA YA 2: USIWASILIANE NAE, JIPE MDA NA NAFASI.
Kuna kitu kinachoitwa ‘no contact rule’ kwa lugha ya wenzetu. Kanuni hii ni rahisi sana na inafanya kazi na yenye mafanikio makubwa. Kitu unachotakiwa kufanya ni kuacha kuwasiliana na mpenzi wako wa zamani kwa mda. Hapa na maana kwamba usimpigie. Kumtumia sms, kuchati nae twiter, facebook,whatsaap na mitandao mingine ya kijamii. Ukiweza futa namba zake kabisa na pia epuka kwenda sehemu ambazo mtaonana.
KWA NINI NISIWASILIANAE NAE?
(    (a) Mpenzi wako wa zamani anahitaji mda na nafasi kusahau maumivu yote baada ya kuachana, na hii itamfanya aanze kukumbuka. Watu wengi wanafikiri kwamba eti kama usipo wasiliana nae atakusahau kabisa, la hasha usipo wasiliana nae unampa mda wa kukumbuka wewe na atakuwa anajiuliza kwa nini haumtafuti?. 
  Hapa unatakiwa ukumbuke yale makosa niliyokuzuia kuyafanya katika hatua ya kwanza. Kitendo chako cha kutomtafuta kinakufanya usionekane mdhaifu bali ngangari na usiye na uhitaji mkubwa.

    (b) Wewe pia unahitaji mda na nafasi, kujitafakari na kujua wapi ulikosea. Unaitaji mda kutafakari kama kuna ulazima wa kurudiana na mtu aliyekuacha au la?Unaitaji kujifunza kama unaweza kuishi bila yeye. Unaitaji mda kujirizisha kuwa unaweza  kuishi ukiwa na furaha bila yeye.Ni kukumbushe kuna msemo usemao “Furaha haiji kwa kupata kitu ambacho huna bali kwa kukipenda kitu ulichonacho. 
(c) Lazima uwe mtu mwenye furaha kwa kipindi hiki cha mpito.
Unaitaji kuyathamini maisha yako kwa sasa. Hii itakusaidia pindi utakapokutana na  mpenzi wako baada ya “no contact period” avutiwe na wewe na kuona kuwa wewe ni mtu mpya.
 NISIWASILIANE NAE KWA MDA GANI? 
Kwa kawaida usiwasiliane nae mpaka pale utakapojiona kuwa umebadilisha maisha yako na unaweza kuendelea hata bila yeye. Kitaalam siku 30 zizatosha lakini unaweza kuchukua hata miezi 2 au 6 kutegemea na sababu zilizowafanya muachane.  
 Kitu cha muhimu hapa kwa kipindi hiki usije ukamwambia kuwa naacha kuwasiliana na wewe kwa mda fulani. Kitendo cha kutowasiliana nae sio ukatili bali ni kwa ajili ya afya ya akili na mwili wako. Kipindi hiki pia usipokee simu zake wala kujibu sms zake.

HATUA YA 3: JIJALI MWENYEWE
Sehemu hii ni muhimu zaidi ndugu yangu ni muhimu sana ndugu yangu. No contact(kutokuwasiliana) hakutakuwa na maana mpaka hapo utakapoamua kubadilsha maisha yako na kuwa bora zaidi. Jijali kwa;
(      (a) Badilisha muonekano wako na kuwa mzuri zaidi. 
   Badilisha muonekano wako, kimavazi kutakufanya uonekane wa thamani zaidi. Unaweza kubadilisha jinsi ya uvaaji, jinsi ya unyoaji ukawa wa kisasa zaidi na unayeendana na wakati. Unaweza kutengeneza mwili wako kwa kufanya mazoezi na kwenda gym. Hapa kuwa makini kidogo usije ukafanya vitu visivyokubalika miongoni mwa jamii inayokuzunguka au ukafanya kitu ambacho uwezi kukisahau kama kuchora tatuu.
(        (b)   Badilisha fikra zako na mawazo yako.
Kuwa mtu mwenye furaha na mwenye kujiamini ni jambo ambalo litakusaidia kurudiana na mpenzi wako. Mpenzi msomaji lazima utambue kuwa furaha ni kitu cha pekee ambachi kinatoka moyoni mwako na akilini pia. Vitu vinavyoweza kukupa furaha ni pamoja na kutoka out na marfiki zako, tembelea kumbi za starehe kama kuangalia sinema, kusoma vitabu vya ujasiria mali na kadhalika.
KWA LEO TUISHIE HAPA USIKOSE HATUA YA NNE.

0 comments:

Chapisha Maoni