Ijumaa, 24 Oktoba 2014

SAIKOLOJIA

KWA NINI WANAUME WENYE SURA MBAYA WANAMILIKI WASICHANA WAREMBO.

 
Hivi ushawahi kujiuliza kwa nini baadhi ya wanaume wenye sura mbaya wanamilki wasichana warembo hapa mjini? Je, ni kweli kwamba wanawake warembo wanavutiwa na wanaume wenye sura mbaya au washambashamba? Kama sivyo, je ni kitu gani cha ziada wanawake wenye mvuto hupenda kutoka kwa wanaume wa namna hii? 

Hivi hushangai kuona mwanaume ambaye hana mvuto anakuwa na msichana mrembo, tena utamkuta mvulana kama huyo yupo kwenye mahusiano mazuri ya kimapeenzi na wewe na u handsomeboy wako upo singe na wasichana warembo wanakukimbia.
Je, ni kitu gani watu wa namna hii wanakuwa nacho na wewe huna? Jibu ni rahisi sana mpendwa msomaji, kwanza wanaume wenye sura mbaya wenyewe hawajifikirii kuwa hawana mvuto, tena isitoshe wao huwa hawafikirii muonekano wao mbele ya wasichana warembo, wao hujiona wapo poa tu na wakati mwingine wanajivunia kuwa wakipekee. 
Hali hiyo ya kujikubali huwafanya wawe wanavaa jinsi wanavyojisikia na kulingana na uwezo wao, hivyo huwa comfortable wanapokutana na wasichana warembo. Sasa wewe unayejifanya handsomeboy utaendelea kusubiri kwa kuwa kila kukicha unawaza uvae nini.

Wanaume ambaye huwa anafikiria kuwa yeye hana mvuto kulinganisha na watu wengine maarufu huwa anajimaliza mwenyewe kisaikolojia na hii umjengea mazingira ya uwoga pindi anapokutana na msichana mrembo. 
Wanaume ambao hawajiamini hutumia nguvu nyingi kufikiria jinsi alivyo badala ya kutumia nguvu hizo kujenga mahusiano na wasichana warembo. Wavulana wasio na mvuto hawatumii mda mwingi kujifikiria na hata wanapotoka out na wasichana huwa kama ni vichekesho kitu ambacho kina create attention kwa wasichana kuenjoy uwepo wao.

Kwa hiyo kitu pekee ambacho ugly guys wanacho ni kujiamini, mvulana hasiyejiamini mara nyingi anajiuliza uliza maswali hivi kweli na mimi na stahili kuwa na msichana mrembo kama yule? Maswali haya huwafanya washindwe kujieleza pindi wanapokutana na wasichana warembo. Wasichana siku zote hawapendi wanaume wasiojiamini.

Kwa nini kujiamini ni silaa zidi ya wasichana warembo? Jibu ni rahisi kwanza lazima tukubaliane kuwa wasichana warembo huwa wanatongozwa mara nyingi na mara nyingi wanaume wanaowatokea ni wale wanaojiamini ni ma handsomeboy na kwa kawaida ya wanume hawa hujaribu kujionesha kuwa wao ni watu wazuri na wenye uwezo wa kuwamiliki. 

Sasa kwa kuwa kila siku msichana mrembo anatongozwa na wanaume wa namna hii basi kwao huwa ni mazoea ukienda na staili hiyo hawaoni jipya kwa kuwa ata jana aliambiwa hivyo hivyo. Wasichana warembo wanataka kitu cha pekee ambacho hawajawahi kuambiwa, kusikia au kuona, wanataka wakutane na mwanaume anayejiamini sio mwoga na pia ambaye anajikubali jinsi alivyo hata kama ni mbaya kiasi gani.

Kujiamini ni silaa kubwa kwa mwanaume anayetaka kumiliki msichana mrembo. Ila kujiamini tu haitoshi mwanaume anatakiwa awe mcheshi, mchangamfu na mkweli vitu ambavyo vitampa nafasi ya kusikilizwa pindi anapokutana na msichana mrembo. 
KWA LEO TUISHIE HAPA. ENDELEA KUFUATILIA BLOG HII UPATE BURUDANI NA MAFUNZO.

LOVE STORY




EVERLASTING LOVE. (Penzi la milele) 
SEHEMU YA 5
MTUNZI: ELIAS ADOLF (eliado)
RACHAEL ANAPATA MARAFIKI
Snoga ana marafiki wengi sana miongoni mwao ni Alex Kijoji huyu ni rafiki yake kwanza wanakaa chemba moja, pili wanasoma kidato kimoja mkondo mmoja na mwaka huo walikuwa form three. Alex yeye anatokea Kondoa Dodoma lakini kwa sasa alikuwa anaishi Dar es salaaam kwa kaka yake. Kaka yake huyo aliamua kumsomesha baada ya baba yao mpendwa kufariki dunia.
Alex anatokea kuwa maarufu sana kwa kuwa na matumizi makubwa sana ya fedha walimpachika jina la B.O.T, kundi lao hilo liliundwa na na yeye pamoja na rafiki yake kipenzi Lucas huyu kweli alikuwa ana hela kwani enzi hizo alikuwa anamiliki simu ya laki tano nae alitokea kondoa japo kwao kabisa ni moshi na familia yao ilikuwa inamiliki mabasi yaendayoamikoani.
Siku moja Snoga na Alex waliamua kushuka huko bondeni yaani bustanini kwa kina Rachael kwenda kuangaza angaza macho, ndipo hapo wanaonana na Rachael na kupata upenyo wa kusalimiana kwani siku hiyo wanafunzi hao walikuwa peke yao bila matron wao. 
Snoga kama kawaida yake alimtambulisha rafiki yake kwa Rachael akitia manjonjo mengi yasiyoitajika. Rachael alifurahi sana kuonana na Alex kwani alitokea kuvutiwa sana na kaka huyo tangia siku nyingi. kilichofuata hapo ni kupanga njia ya kumpata mtanashati huyu lakini kazi ilikuwa ngumu kwani mtu ambaye hamjazoeana ni kazi sana kumwingiza mtegoni. Shughuli ilianza kwani usiku kucha Rachael hakulala kwa kumwazia Alex na hata alipopata usingizi bado alimwota tena ndoto pevu, alipoamka picha ya Alex ilimjia machoni mwake, basi taratibu alijikuta akikosa raha siku nzima.
 Baada kama ya siku tatu Rachael akapatwa na ugonjwa wa malaria, ingawa kiukweli haikuwa malaria bali msongo wa mawazo na akalazwa katika dispensary iliyopo hapo hapo mission.

Snoga aliposikia Rachael amelazwa, aliamua kwenda kumwona lakini safari hii hakuwa na ALEX alikuwa na rafiki yake mwingine, Rachael alifurahi sana na kitu cha kwanza kuuliza ilikuwa rafiki yake yukwapi yaani ALEX. 
Snoga akamwambia nilimwacha ana shughuli nyingi pale shuleni kwani siku hiyo ilikuwa ya usafi na yeye ni kiongozi tena wa afya hivyo alikuwa anasimamia usafi. Rachael alikasirika moyoni ingawa hakuonesha usoni, wanafunzi hawa wa Kwiro walipoaga kitu muhimu walichosisitizwa ni kwamba wasisahau kumwambia Alex aende kumwona. 
Snoga baada ya kufika shuleni alifikisha ujumbe alopewa ingawa kwa shingo upande kwani alishaanza kuhisi kuna kitu kilikuwa kimejificha haiwezekani watu wamejuana siku moja tu tena kwa mgongo wangu alafu auliziwe hivyo. Ujue kwa uzuri wa Rachael kila mwananaume alitaka kuwa nae sasa kilchomsumbua Snoga ni wivu na tamaa.
Siku iliyofuata Alex alikwenda kumsalimia Rachael akajikuta bila kutegemea kwa mara yake ya kwanza maishani anabeba kadi ya pole, soda, biscuit na matunda kwenye kilasketi chake ambacho huwa kinawachengua watu hasa maduu pindi akivaapo. Alipooingia tu wodini Rachael aliinuka ghafla na kukaa huku mapigo ya moyo wake yakiongezeka. 

Alex alifanikiwa kuigundua hali hiyo lakini hakushangaa sana, walipiga stori nyingi sana ikiwa ni pamoja na kutambulishana vizuri. Rachael alijitambulisha kuwa yeye anatokea masaki jijni Dar, na Alex nae akasema anatokea huko huko Dar yaani manzese. Ilikuwa zaidi ya furaha kwa Rachael kusikia pia jamaa anatokea Dar na kwa haraka alipiga hesabu kuwa ifikapo likizo watakuwa wote Dar.
 Rachael akamwambia Alex kuwa siku iliyofuata atatoka na hivyo ataenda likizo ya wiki moja ili akapumzike kwa Babu yake hapo mahenge.
Ikumbukwe kuwa asili ya Rachael ni mpogoro wa mahenge ingawa wazazi wake wapo DAR, ila huku ni kwa marehemu babu yake Mbunda wa Mbunda. Hivyo alimwomba Alex kuwa pindi atakapotoka na kuchukua ruhusa ya wiki waonane nyumbani kwa babu yake kwani ana mazungumzo na yeye hivyo aende peke yake.
Alex alikubali lakini alimwomba wafanye keshokutwa kwani kesho angekuwa bize sana na mambo ya shule na kuanzia saa nane mchana yaani baada ya vipindi vya darasani anatakiwa aende benki kuchukua hela ya matumizi.
 Rachael kusikia hela ya matumizi akamwambia kwa hilo asiwe na hofu hiyo hela ya matumizi ilipo banki aiache tu kwani yeye atampa zingine. Alex alishangaa sana kusikia hivyo kwani hela alizotaka kwenda kuzichukua ni nyingi hivyo akamwambia tena itanibidi niende tu kwani hela ninazotaka kuzichukua ni nyingi sana yaani ni pamoja na ada ya shule. Lakini cha ajabu na kushangaza Rachael kwa kiburi na dharau akamwambia hata ingekuwa ya nini bado angempa.
Hapa inanikumbusha nilipokuwa nikisoma mimi jirani yetu kulikuwa na shule ya private wao walikuwa wakilipa milioni kwa mwaka alafu sisi elfu sabini hivyo walikuwa wakitudharau sana wakidai ada yetu ni sawa nahela yao ya matumizi kwa mwezi. Hapo Alex hakuwa na cha kujitetea tena zaidi ya kukubali matokea na kutii ratiba ya Rachael.
Basi Alex aliporudi shuleni kwao akawapatia wenzie stori ya yaliyori huko hospitalini, watu wakacheka na kufurahi sana na kila mtu alijaribu kutoa ushauri wake, wapo waliosema ”kamatia hapo hapo mwanangu na wengine walisema hafai kutokana na skendo zake kwanza usikute ana ukimwi anausambaa kwa watu.” basi kila mtu alisema lake siunajua tena kwenye wengi pana mengi lakini binafsi Alex aliamua kwenda kumsikiliza mrembo huyo.

Kesho ilifika na Alex alitimiza ahadi yake kwa kufika kwa kina Rachael tena kwa mda waliokubaliana, alimkuta Rachael akimsubiri kwa hamu na jam, akakaribishwa sebuleni na siku hiyo ndugu zake Rachael hawakuwepo kwa mda huo bali kulikuwa na watoto wadogo ambao wasingeweza kuathiri mazungumzo ya wawili huo. 
Walizungumza mengi lakini kubwa na la muhimu lilikuwa bado limefichwa. Kama kawaida yake binti huyu mwenye hulka za kizungu alianza kutoa ya moyoni. 
Alianza kwa kusema “Alex kuna kitu kimoja kinanisumbua sana ndani ya uvungu wa moyo wangu, nmejitahidi kuvumilia lakini kila nikikuona mwili wangu unakufa ganzi, nmeona nkwambie ukweli tu japo maadili ya kiafrika hayaturuhusu kufanya hivyo. kiukweli ntapata nafuu kama utanirusu nisogee karibu yako zaidi nkwambie ninachotaka kukuambia. ‘Alex alisita kidogo lakini akamwambia wewe endelea tu nakusikilia..
Rachael akaendelea kusema 'mwenzio tangia nilipokuona ile siku ya kwanza nilihisi mapigo ya moyo kwena mbio na baadhii ya sehemu zangu kusisimuka ajabu, msisimko ulionipelekea kupata upweke wa ghafla, ila kuna kitu kimoja kinachonifurahisha na kunifariji kutoka kwako na hii ni mara baada ya kufanya uchunguzu wangu na kuwauliza rafiki zako kuhusu wewe wakanieleza kuwa wewe ni mtu mzuri sana, mstaarabu, mpole na usiyependa shari na kikubwa aidi wewe ni handsomeboy.
 Kwa kweli umetokea kuuteka moyo wangu kwa mda mfupi sana, nashindwa kujieleza zaidi kwani nahisi kurudiarudia maneno ila ninachokuomba Alex mpenzi fungua moyo wako unipatie pumziko la milele kwani nmechoshwa huko ntokako please. 
ALEX naomba unielewe nakupenda sana, sauti hiyo ilitoka kwa shida sana nahisia nzito ikiambatana na kwikwi zilizomsababishia Alex kuwa kimya kama yupo kanisani alitamani akatishe maneno kwa kusema na yeye anampenda lakini kukawa na sauti mbili inaopingana ndani ya moyo wake.
Alex baada ya kuona Rachael amekaa kimya na kusubiri jibu aliamua kuvunja ukimya kwa kusema”kwa sasa sina jibu la kukupa kwa sababu sikulitegemea hilo” Rachael hakuridhika ikabidi amuulize anachoogopa ni nini ili hali yeye sio mtoto kama kuna kitu unaogopa niambie na mimi nikijue au una girlfriend mwingine?. Alex akamwambia hapana ila nashindwa kuamini msichana mzuri kama wewe usiwe na boyfriend au ndo unataka kutuchanganya.
Rachael kwa sauti ya unyonge ”hapana my dear ila sijui nikuelezaje mpaka unielewe,mimi niko mwenyewe nielewe mwana wa mwenzio niepukane na hichi kilio, please nikubalie basi niondoke kwenye ulimwengu huu wa upweke, safari hii Rachael alisimama na........................................................... USIKOSE SEHEMU YA SITA

Alhamisi, 23 Oktoba 2014

UHUSIANO



JINSI YA KUFANYA MWANAMKE AJISIKIE SPECIAL
 
Hakuna mwanaume hasiyependa mchumba wake, mkewe au girlfriend wake ajisikie special. Hivi unajua ni kwa kivipi? Acha leo nikueleze ni nini hasa mwanamke anahitaji and how real men can make it. Zifuatazo ni njia mbadala
(1) JUA NINI ANAHITAJI
Ni ukweli wa asili (fact of nature) kwamba wasichana huwa wanahitaji kitu fulani kutoka kwa mwanaume. Najua ni ngumu kwa mwanaume kujua vitu hivyo kwa sababu vipo ndani ya ya mioyo ya wasichana. 
Huwezi kuepuka ukweli huu, cha msingi mwanaume anatakiwa kujifunza na kujua nini mwanamke anahitjai kutoka kwake, kwa hiyo ukijua kwa undani au kwa kiasi kikubwa nini msichana anahitaji ndivyo ilivyo rahisi kumfanya yeye ajisikie special. 
Ni ukweli usiopingika kwamba sio wasichana wote wanafanana kwa vitu wanavyohitaji lakini cha msingi ni kujua how women act, think and feel when they are in love. Zifuatazo ni vitu ambavyo msichana akifanyiwa ujisikia special.
(a)Wasichana wengi wanapenda utulivu
Hivi unajua ni kwa nini wasichana wengi hawapendi kwenda bar, na badala yake wanapendelea kenda parties ambapo wanaweza kukutana na watu wa aina mbalimbali. Ni makosa ya wanaume wengi kwani wao ufikiri kuwa bar ni sehemu nzuri ya kukutana na mwanamke (hapa ndugu zangu wanywaji mnisamehe). 
 
Ukweli ni kwamba wanawake wengi hupenda kujikita kwenye vitu ambavyo vitakuza vipaji vyao, vitaongeza thamani yao katika jamii, kwa hiyo kama msichana anapenda movies basi mpeleke sehemu wanazoonesha sinema na kama anapenda pombe basi mpeleke bar (hapa ngugu zangu walevi tugonge cheers). Msichana siku zote hujisikia special ukimfanyia kitu anachokipenda na pia umweka huru zaidi.
(b) Je, vipi kuhusu wasichana wanaopata care nyingi kutoka kwa wanaume?
Kundi hili ni la wasichana ambao ni warembo kupita kiasi na kutokana na uzuri wao wameshazoea kufanyiwa vitu ambavyo vinawapa utulivu. Sasa hapa ni tofauti kidogo, kama unataka kumfanya ajisikie special msichana wa namna hii try to treat her as normally as possible, kwa sababu utakapo mpeleka sehemu alizozoea kupelekwa au utakapomfanyia vitu alivyozoea kufanyiwa sana kimoyomoyo atajisemeha huyu nae ni walewale hana jipya. 
Kwa hiyo kwa sampo hii jitahidi kwanza kumfanya ajisikie huru kwa mfano unawweza kumjengea mazingira kuwa unamwona kama dada yake, unamweshimu sana na pindi utakapokuwa nae jaribu kuwa fan and joking. Mchekeshe mfurahishe na ikiwezekana mtanie.
(c) Njia rahisi za kumfanya ajisikie special
Mwanaume hautaji kutumia mda na hela nyingi kumfanya msichana ajisikie special viyu vidogo vidpgo tu vinatosha kwa mfano unaweza kumtumia sms asubuhi, mchana na jioni hii inatosha kumfanya aone unamwaza kila wakati kwa hiyo yeye ni special. 
Pia unaweza kumuuliza kuhusu siku yake ilivyoeenda hii mara nyingi ni mda wa usiku kabla hajalala, hapa utapata nafasi ya kuanzisha mazungumzo mengine na pia atajua kuwa unayapenda maisha yake.Kitu kingine ambacho ni rahisi zaidi ila kina madhara kama hutokitilia maanani ni ‘promise’ keep your promise kwa kila kitu ulichokisema hapa atajisikia special.
(2)MFANYE AJISIKIE UNAMPENDA
Hapa niwaachie wasomaji, ebu niambie kwa mtazamo wako njia au vitu vya kufanya ili mwanamke ajione unampenda.... kazi kwenu ila msisahau kipimo cha ulijali hakipimwi kwa kulala na wanawake wengi la hasha manhood is measured by how well a man can love a women.

LOVE STORY




EVERLASTING LOVE (Penzi la milele)
SEHEMU YA 4
MTUNZI: ELIAS ADOLF(eliado)
ILIPOISHIA
Wazazi wake Rachael wamerudi kutoka Arusha walipokuwa wakienda mapumzikoni na hii ni baada ya kupata taarifa za msiba wakiwa njiani, mama yake Rachael anaingia chumbani kwa mwanaye na kukuta Rachael yupo juu ya mwanaume wakivunja ile amri ngumu ya sita..Tiririka....

Basi watafanya nini hili hali mtoto akiunyea mkono huwezi kuukata, wanamgombeza sana na Emmanuel anatishiwa kuuwawa na bastola na baba yake Rachael lakini kwa huruma ya mama Rachael anafanikiwa kumtoa nje na kumwambia apotee eneo hilo haraka.
Majuto ni mjukuu, roho inamuuuma sana Emmanuel lakini hana jinsi maji yakishamwagika hayazoleki, kichwa chini, mikono kichwani utamu umegeuka shubiri, anafika kwao anapokelewa na maneno makali sana kutoka kwa mama yake mkubwa siunajua tena mtoto huyu yupo masomoni jijini hapa nyumbani kwao ni kule Dodoma.
Huku nyuma baba na mama yake Rachael wanapanga kumwamisha shule mtoto wao kutokana na matukio yanayoendelea kutokea, kimoyomoyo walikuwa wakiyakumbuka maneno wa marehemu Mbunda wa Mbunda aliyetabiri juu ya maisha ya huyu mtoto lakini imani ya dini iliwafamya kujisahulisha.
 Rachael alichanganyikiwa kwa penzi la mtoto wa askofu na hata wazazi wake walijiuliza sana bila kupata jibu. 
Walishauriwa na mwalimu wa malezi kuwa wasubiri mwaka huo uishe kwani zilbaki wiki tano tu kabla ya kumalizika kwa muhula wa pili ili atakapohamia akaanze kidato kingine, bila kinyongo walikubaliana na ushauri huo na walimsihii Rachael ajitaidi kufanya vizuri. 
kwa hiyo ndani ya mwezi huo mmoja watoto hawa wadogo lakini wenye mambo makubwa waliendelea na mahusiano yao ya kimapenzi kama kawaida. Sasa hivi walibadili staili ya kulimenya tunda walikuwa wanasubiri wikiendi na wanakwenda kwenye nyumba za wageni na kufanya utundu wao.
Baada ya mwezi ule wa mitihani kumalizika Rachael alikuwa anasubirri ifike january ya mwaka mwingine apate kuama shule kwani hata yeye ingawa alikuwa akimpenda sana Emmanuel lakini alikuwa amechoshwa na malalamiko ya wazazi, waalimu na wanafunzi wengine kuwa yeye hajatulia, akijaribu kulinganisha na uvumi uliozagaa wiki moja kabla ya mitihani eti yeye aligawa penzi kwa mwalimu wa hesabu ili apewe majibu. 
Roho inamuuma sana kwani zile zilikuwa njama zilizopangwa na Juliet msichana aliyetokea kumpenda sana boyfriend wake. Kwa kiasi kikubwa skendo hii ilifanikiwa kwani Emmanuel hakuwa tayari tena kuendelea na Rachael na likizo hii aliamua kurudi kwao Dodoma kuwasalimia wazazai wake.

RACHAEL AHAMIA SHULE MPYA
Tarehe 13/01 Rachael anaripoti katika shule ya wasichana iliyopo morogoro wilayani mahenge ulanga, shule hiyo iitwayo ST AGNESS GILRS SECONDARY SCHOOL iliyo chini ya parokia ya kwiro jimbo la mahenge pia chini ya muhasham baba askofu Agapty Ndorobo. 
Shule hii ni nzuri kiupande wa maadili kwani watoto wa pale wanalelelwa katika misingi ya kidini. Rachael anapokelewa na na matroni Maria ambaye ndio sister mlezi wa shule hiyo pia anakabiziwa kwa mwanafunzi mwenzake kama mwenyeji wake aitwaye LUCY MASIMBI huyu wanatokea kuzoeana sana kutokana na uchangamfu wake.
Maisha yanaendelea vizuri kwa Rachael japokuwa inaonekana kama ngumu kwake kwani kuamka ni saa kumi na moja na ifikapo saa kumi na mbili wanafunzi wote wanatakiwa wawe kanisani haijalishi ni muislamu au mkristu, maadam upo pale unatakiwa kufuata shughuli na ratiba za pale.
 Na kila saa sita mchana na saa kumi na mbili jioni watu wote husimama na kusali ile sala ya malaika wa bwana kwa wale waamini wa kikatoliki wanajua sala hiyo. Masomo yanaanza kama kawaida saa mbili asubuhi na ifikapo jioni kuanzia saa kumi na moja jioni huwa wanakwenda bustanini iliyo kidogo chini ya shule hiyo basi huko ndipo Rachael huwa anafurahi.
 kwani hupata nafasi ya kuonana na wanaume au wavulana ingawaje huwa hapati nafasi ya kuongea nao lakini kwake huwa ni zaidi ya faraja. 
Sehemu hiyo kuna uwanja wa mpira wa miguu hapo huwa wanafanya mazoezi wavulana wa aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na wale wa shule ya wavulana iitwayo Kwiro boys high school, hii ni shule kongwe iliyoanzishwa na wajerumani na watu wengi maarufu walishawahi kusoma hapo.
Zamani ilijengwa kwa makusudi ya kidini lakin mwaka 1967 iliitaifishwa na serikali, ina wanafunzi wengi sana na wanatoka karibu mikoa yote ya nchii hii , inasifika kuwa na mahabara nzuri sana licha ya hayo mazuri pia ina sifa kubwa ya kuwa na fujo na vurugu. 
Miaka ya nyuma iliripotiwa wanafunzi wa hapo walishawahi kuchoma mabweni na kupiga mawe msafara wa mkuu wa wilaya. Kwa hiyo hata hiyo shule ya kina Rachael walikuwa wakiwaogopa sana.
Kuna baadhi ya wanafunzi wa shule hizi mbili walikuwa na mahusiano mazuri ya kiuwanafunzi lakini wengine wao ni mapenzi tuu na kusahau kilichowapeleka huko. 
Kuna mwanafunzi mmoja jina lake Resty huyu alikuwa na kaka yake hapo Kwiro secondary waliishi kwa raha sana na kila siku walikuwa wakionana kisiri na kusalimiana, kaka yake huyo alipata umaarufu sana kutokana na the way jinsi alivyo alikuwa tozi sana na muongeaji sana kwa hiyo alijuana na mabinti wengi sana wenyewe walimwita SNOGA, huyu jamaa alikuwa na kipaji cha kucheza ile miziki ya kizungu kama vile hana mifupa hapa huwa namkumbuka marehemu Michael Jackson. 

Kwa kuwa Rachael alikuwa anatamani sana kupata rafiki wa kiume kutoka kwenye shule hiyo, alianza kazi hiyo mara moja bila mafanikio baadae alipotafakari sana aliona kuwa kulikuwa na aja ya kuunda urafiki na Resty dada wa yule tozi (Snoga bowow). Kwa kuwa siku zote penye nia pana njia, Rachael alifanikiwa kuwa na urafiki na Resty, lakini kwa mda mfupi tu Resty alifanikiwa kuisoma vizuri tabia ya rafiki yake na kugundua kuwa sio nzuri.
 
Kwani ni juzi tu Rachael alishafanikiwa kumwingiza mfanyakazi wa shule yaani mtunza bustani katika himaya yake ya utumwa wa mapenzi na kumsababishia mvulana huyo kufukuzwa kazi kwa madai ya kuwa na ukaribu na baadhi ya wanafunzi wa hapo.
Kwani alishawahi kufumwa na Rachael huko bustanini wakifanya vitu vya ajabu, sitaki kulielezea sana tukio hili kwani vitu vya Rachael si mnavijua ana maufundi ya ajabu. 
Alifanikiwa kuwa karibu sana na Snoga lakini alishindwa kumuingiza kwenye himaya yake kwa sababu mtanashati huyu alishaonywa na dada yake juu ya tabia mbaya ya Rachael. Ingawa kwa upande wake aliona kama anazibiwa bahati tuu, na alijisemea kimoyomoyo kuwa akiingia anga zangu kwa uzuri aliokuwa.................

Jumatano, 22 Oktoba 2014

DARASA LA MAPENZI



ZIFAHAMU FAIDA ZA KUFANYA MAPENZI

Kila kitu dunian kina faida na hasara ingawa wengi wanazani kuwa tendo la ndoa ni kwa ajaili ya kujifurahuisha tua au kuzaliana. Ni weke wazi lengo langu si kuhamasisha watu wafanye ngono kwani ukimwi upo na unauwa. Wataalam wa mambo ya afya wamefanya utafiti na kugundua kuwa zipo faida za tendo la ndoa au kufanya mapenzi kwa maneno mengine kama tu yatafanywa kwa utaratibu maalum. Zifuatazo ni baadhi ya faida.

Kiafya.
Wataalam au wanabailojia wanadai kuwa kufanya mapenzi ni moja kati ya mazoezi ya mwili. Endapo mtu atafanya tendo hilo mara tatu kwa wiki kwa mda wa mwaka mzima ni sawa na kukimbia mail 75. Kama watu wakifanya mapenzi kwa mda wa nusu saa tendo hilo uongeza vizalisha nguvu 150 na hii ni sawa na kukimbia dakika 15 kiwanjani. Kwa hiyo tendo la ndoa ni mazoezi tosha kwa mwanadamu kama atalifanya kwa utaratibu.

Kuongeza msukumo wa damu.
Kufanya mapenzi husaidia kuongeza kasi ya mtiririko wa damu kwenye ubongo na sehaemu nyingine ya viungo vya mwili na hii huchangia kuongeza kasi ya mapigo ya moyo na kupumua ambavyo huboresha mzunguko wa damu mwilini.

Kadri kiasi cha damu mpya mpya yenye oxegen na homoni inapofikia chembechembe za damu, viungo na misuli inatumika katika zoezi la uunguzaji wa chakula na damu iliyotumika inapoondolewa, pia kiasi cha uchafu hutolewa ambacho ungesababisha misuli kushindwa kufanya kazi na hivyo kusababisha maumivu ya mwili.

Hupunguza mafuta yenye kileo (Cholesterol).
Kufanya mapenzi kwa mpangilio kutakusaidia kuweka sawa uwiano wa mafuta yenye kileo(Cholesterol) nzuri na cholesterol mbaya na wakati huo huo hupunguza kwa ujumla kiasi cha mafuta yenye kileo mwilini.
Kupunguza maumivu.
Wakati wa kufanya mapenzi homoni iitayo Oxytosin huzalishwa mwilini ambayo husababisha kuzalishwa kwa homoni iitwayo Endrorphin ambazo husaidia kupunguza maumivu kama vile kuvimba sehemu za viungo(Arthritis) maumivu ya shingo (Whiplash) na maumivu ya kichwa, kiuno na mgongo. Hivyo basi unaweza kujitibu mwenyewe magonjwa yaliyotajwa hapo juu sio kukimbilia kunywa dawa.

Hupunguza baridi na mafua.
Wataalam wanasema kuwa wanaofanya tendo la ndoa mara moja au mbili kwa wiki huonesha 30% ngazi ya juu ya ulinzi wa mwili uitwao Immunogloulin, ambayo inaongeza kinga mwilini.

Kuonekana kijana na kuishi mda mrefu.
Wataalamu wanabainisha kuwa wakati wa tendo la ndoa kuna homoni iitwayo Dhea huzalishwa. Hii husaidia msisimko wa mapenzi kuongezeka. Dhea ni kemikali ambayo husaidia kuweka sawa kinga ya mwili, huongeza hufahamu, kuimarisha mifupa, kuimarisha afya na mishipa ya moyo (Cardiovascular) na pia hufanya kazi ya kulinda mishipa ya fahamu.

Huongeza uzalishaji wa Homoni za kike (Oestogen) na za kiume (Testosterone).
Kufanya mapenzi kwa mpangilo maalumu huongeza uzalishani wa homoni tajwa hapo juu ambazo huimarisha mifupa na misuli. Madaktari wanabainisha kuwa homoni za kiume huufanya moyo uwe na afya na kuwa na mafuta yenye kileo (Cholesterol) mazuri kuwa mengi, kwa wanaofuatila zaidi nshataja kazi yake hapo juu. Tendo la ndoa humwongezea mwanamke homoni ya kike(Oestrogen).
kutunza tissue za sehemu ya uke na pia kuulinda mwili zidi ya magonjwa ya moyo. Homoni hii umwongezea mwanamke hisia hivyo kuwajibika vizuri wakati wa tendo la ndoa.


 

KWA LEO TUISHIE HAPA, USIKOSE DARASA LA MAPENZI LA KESHO.